Tetesi za soka Ulaya leo Ijumaa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
UPANUZI wa uwanja wa ndege wa Barecelona hautawezekana kwa sababu "ndege haziruhusiwa kupaa juu ya nyumba ya Lionel Messi "kwa mujibu wa Rais wa Vuielig Javier Sanchez-Prieto. (Marca)
Lionel Messi
Meneja wa Austria Franco Foda anatazamia kumchukua mashambuliaji Ashley Barnes. Aliwahi kuchezea Austria mwaka 2008 kwenye timu ya under-20 (Austria Press Agency, via Sky Sports Austria)
Manchester United wanuangana na Liverpool katika kumtafuta kiungo kutoka Napoli Jorginho, 26, meneja Jose Mourinho akiwa tayari kulipa paundi milioni 50 kwa ajili ya nyota huyo Muitaliano(Star)
Wakala wa Mario Balotelli anasema mchezaji huyo aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester City na Liverpool,aweza rudi majira ya joto na kucheza katika Ligi ya Premier (Mirror)
Mkuu wa West Ham David Moyes anaandaa paundi milioni 10 kumnadi mchezaji Harry Arter baada kushindwa kumpata kiungo huyo mara mbili kabla (Express)
West Ham wana mipango kumpatia dili mpya kiungo wa Argentina Manuel Lanzini, 25, ilikupoteza Liverpool wanaomtaka pia. (Evening Standard)
Mazungumzo juu ya mkataba mpya kati ya Courtois na Chelsea yamesukumwa mbele hadi majira ya joto (Sun)
Liverpool wanatazamia kumsajili kiungo wa Southampton kutoka Gabon Mario Lemina. (L'Equipe)
Tottenham wako tayari kumchukua mshambuliaji Mjerumani Marco Reus,28, wa timu ya Borussia Dortmund (Mirror)
Timu za Paris St-Germain na Real Madrid wanamvizia mlinda mlango wa Chelsea Thibaut Courtois,25. Baba yake Thibaut alikutana na timu hizo kwa mazungumzo yasiyo rasmi wiki hii (RTBF, via London Evening Standard)
No comments:
Post a Comment