Viongozi 12 ACT-Wazalendo wang'atuka wajiunga CCM....soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

VIONGOZI 12 katika ngazi mbalimbali wa Chama cha ACT-Wazalendo wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Dar es Salaam wamejivua uanachama na kuhamia CCM wakimtuhumu Zitto Kabwe kutoa matamko kinyume na misingi ya chama.
Aliyekuwa mwenyekiti ACT-Wazalendo mkoa wa Dar es Salaam, Ernest Kalumuna akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wengine ni viongozi ngazi mbalimbali waliohamia CCM.

Kujiondoa huko kumetangazwa leo na Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Dar es Salaam, Ernest Kalumuna alipokuwa akiongea na waandishi was  habari kwa niaba ya wanachama hao 12 kuelezea sababu za kukihama chama.

“Tumeshtushwa zaidi na kauli za karibuni za kiongoz wa chama ndugu Zitto Kabwe kuhamasisha viongozi wa Chadema wakae na kufanya maamuzi ambayo anadai sisi tutawaunga mkono huku akimalizia kwa kusema serikali hii ni rahisi kuiangusha,” amesema Kalumuna.

Amesema matamko hayo ni ishara kuwa kiongozi huyo amefilisika kisiasa na kueleza kitendo cha  kamati kuu ya chama kushindwa kukutana na kutoa tamko la kupinga kauli hizo inamaana sasa chama hakina kamati kuu na hivyo chama kinaongozwa na mtu mmoja na wapambe wake.

Amesema  kwa sasa chama hicho kina hali mbaya na hakileti matumaini ya kuwa  chama mbadala kama kilivyojinasibu awali

Viongozi waliohama
Ramadhan Ramadhan- Makamu Mwenyekiti Taifa Zanzibar wa kwanza mwanzilishi aliyeandikisha chama kwa msajili, Leopold Lucas Mahona-Naibu katibu mkuu Bara wa kwanza wa ACT aliyeandikisha chama kwa msajili, Hudson Mwakyambiki-Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya chama.

Wengine ni Ernest Theonest Kalumuna-Katibu wa chama mkoa wa Dar es Salaam, Mikidadi Ramadhan Kirungi-Katibu jimbo la Ubungo, Khalfan Sadadi-Katibu jimbo la Kibamba, Sadich Mohamed Msangi-Katibu Mwenezi Jimbo la Kibamba.

Pia wamo Swaumu Hamisi Msipu-Mwenyekiti Ngome ya wanawake Jimbo la Ubungo, Robert Kihiri-Mwenyekiti Ngome ya vijana jimbo la Ubungo, Mtangi Hatibu semwanza-Mwenyekiti wa kata ya Manzese jimbo la Ubungo na mgombea udiwani kata ya Manzese 2015 na Ally Hamis Semwanza-Katibu wa chama kata ya Manzese jimbo la Ubungo.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search