UDSM yamsimamisha masomo Abdul Nondo.... soma habari kamili na matukio360....#share

Na mwandishi wetu, Dar es salaam
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. William Anangisye, amemsimamisha masomo Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi kesi yake ya kudanganya kuwa alitekwa na kuchapisha taarifa za uongo mitandaoni itakapomalizika.
Uamuzi huo unatolewa baada ya Jana Machi 26, Nondo kuachiwa baada ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia kutoa maamuzi kuwa dhamana ipo wazi na mtuhumiwa huyo kutimiza masharti ya dhamana.
Masharti ya dhamana ni kudhaminiwa na watu wawili ambao ni wakazi wa Iringa, huku mmoja awe mfanyakazi wa serikali, na wanatakiwa waweke bondi ya Sh. 5 milioni sambamba na kuwa na mali isiyohamishika, ambayo Nondo ameyatimiza na kupata dhamana.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. William Anangisye, amemsimamisha masomo Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi kesi yake ya kudanganya kuwa alitekwa na kuchapisha taarifa za uongo mitandaoni itakapomalizika.
Uamuzi huo unatolewa baada ya Jana Machi 26, Nondo kuachiwa baada ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia kutoa maamuzi kuwa dhamana ipo wazi na mtuhumiwa huyo kutimiza masharti ya dhamana.
Masharti ya dhamana ni kudhaminiwa na watu wawili ambao ni wakazi wa Iringa, huku mmoja awe mfanyakazi wa serikali, na wanatakiwa waweke bondi ya Sh. 5 milioni sambamba na kuwa na mali isiyohamishika, ambayo Nondo ameyatimiza na kupata dhamana.
Kesi ilihairishwa hadi Aprili 4, 2018 itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili, la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.
Shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma mjini Mafinga alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha Polisi Mafinga kuwa alitekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam na kupelekwa Kiwanda cha Pareto cha Mafinga.
No comments:
Post a Comment