Yanga yaichapa Kagera Sugar 3-0...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

TIMU ya Yanga imeendelea kuisogelea timu ya Simba kwenye msimamo wa ligi katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom baada ya kuibuka na ushindia wa goli 3-0 dhidi ya Kagera Sugar.

Mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaa, umeshuhudiwa magoli hayo yote yakifungwa  kipindi cha pili ambapo goli la kwanza limefungwa  na Ibrahim Ajibu kwa mkwaju wa penati huku la pili likifungwa na Yusuph Mhilu na latatu Kagera Sugar wakijifunga.

Ushindi huo unaifanya Yanga kuwa nyuma ya mtani wake wa jadi Simba kwa  pointi tatu kwani Simba iko kileleni mwa msimamo kwa pointi 46 huku Yanga ikiwa na pointi 43 huku timu zote zikiwa zimecheza mechi 20.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search