Makonda awajibu wanaobeza kampeni ya akina mama waliotelekezwa...soma habari kamili na matukio360..#shar
Na Mwandishi Wetu, Dar
es Salaam
MKUU
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wale wote wanaosema kampeni yake
ya kuwasaidia akina mama waliotelekezwa na watoto imevunja sheria, pengine wana
watoto nje na wanaogopa kujitokeza.
Makonda ameyasema hayo leo Aprili 19, katika uzinduzi wa
hospitali ya kisasa ya mama na mtoto iliyopo Chanika iliyojengwa kwa msaada wa
Shirika Maendeleo la Kimataida la Korea (Koica).
“Eti wanasema navunja sheria, natakiwa nifanye faragha kama
unataka faragha tunza mtoto. Mimi siogopi, nipo tayari kufungwa lakini kwa
ajili wa kutetea haki za watoto. Pengine hao wanaosema navunja sheria wana
watoto wao nje wanaogopa kujitokeza,” amesema.
Jana, Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba
Kabudi akiwa bungeni alisema kampeni hiyo inaweza kuleta hali ya
sintofahamu na akabainisha kuwa inapaswa kufanyika faragha na sio kama
inavyofanyika sasa.
Awali, Waziri wa Afya, Jinsia, Wanawake na Watoto, Ummy
Mwalimu alisema kampeni hiyo ni sahihi ila kasoro yake ni kutokuwa na faragha,
lakini akasema kwa sasa inafanyika huku picha za watoto zikifichwa.
Aliyeibua hilo bungeni jana alikuwa ni mbunge wa Ulanga,
Goodluck Mlinga aliyehoji uhalali wa kampeni hiyo na akahoji kama haivunji
sheria na kuwavunjia haki wanawake na watoto.
No comments:
Post a Comment