TCAA yaagizwa kusimamia usafiri wa anga...soma habari kamili na matukio360...#share
Na
Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, ameitaka Mamlaka ya Usafiri wa
Anga Tanzania (TCAA), kusimamia usafiri wa anga kwa kuzingatia taratibu na kanuni
za usafiri huo ili kuweka uwiano wa haki kwa waendeshaji na abiria wanaotumia
usafiri huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,
Profesa Makame Mbarawa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya
Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) lililofanyika mjini Dodoma.
Ametoa kauli hiyo mjini
Dodoma wakati akizindua rasmi Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo na
kuwapongeza kwa kuamua kuweka mikakati ya kununua rada nne kwa kutumia fedha za
ndani.
“Lazima msimamie kanuni
na taratibu zilizopo, wajibu wenu ni kutoa haki kwa watumiaji na abiria kwa
usawa, hatutaki kusikia mnakandamiza watumiaji wa usafiri na mkisimamia vizuri
eneo hili mtafanya idadi ya watumiaji kuongezeka na makampuni kuendelea kuwekeza
zaidi kwenye usafiri” amesisitiza Prof. Mbarawa.
Waziri Prof. Mbarawa
amesema yeyote anaevunja taratibu zilizowekwa kwenye usafiri wa anga Mamlaka
hiyo ichukue hatua stahiki kulingana na taratibu zilizopo ili usafiri huo uweze
kuwa na nidhamu.
“Kila Kampuni mkiiachia
ifanye inavyotaka hatutafika popote na malalamiko kwenye usafiri wa anga
yataendelea kuwepo, hivyo naomba msimamie makampuni haya kwa ukaribu mkubwa,’
amesisitiza Prof. Mbarawa.
Ameongeza kuwa ili
mamlaka ifikie lengo na kufanikiwa lazima Menejimenti ishirikishe watumishi kwa
karibu ili kutimiza malengo iliyojiwekea.
Prof. Mbarawa amesisitiza
umuhimu wa TCAA kuwawezesha watumishi wake kitaaluma na kimaslahi ili kuongeza
tija katika kazi na kufikia malengo ya utendaji Kitaifa na Kimataifa.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Bw, Hamza Johari, amemhakikishia Waziri Prof.
Mbarawa kuwa TCAA imejipanga kutekeleza miradi mbalimbali kwa kutumia vyanzo
vya ndani ili kuvutia makampuni ya ndege ya ndani na nje ya nchi.
“Nikuhakikishie kuwa
tumejipanga kutekeleza miradi mingi zaidi kwenye usafiri wa ndani ili kuchochea
kasi ya usafiri huo lakini pia kutimiza amza ya kuboresha usafiri huo, ”amesema
Johari.
Ameongeza kuwa kwa sasa
mamlaka iko kwenye hatua za awali za utekelezaji wa mradi wa kufunga vifaa
maalum vya kuwezesha ndege kwa usalama katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa
cha Zanzibar ambapo mradi huo ukikamilika utaimarisha huduma za kuongozea ndege
katika kiwanja hicho.
No comments:
Post a Comment