Miguna Miguna asafirishwa kutoka Dubai kwenda Canada...soma habari kamili na matukio360...#share
Miguna Miguna
Bw Miguna Miguna, ambaye ni
wakili, amesafiri kwa ndege iliyokuwa ikielekea Toronto, Canada, baada ya kukaa
katika uwanja wa kimataifa wa Dubai kwa siku nne.
Gazeti la Nation, limesema
afisa mmoja wa serikali amewafahamisha kwamba Bw Miguna aliondoka Dubai
akitumia ndege ya Air Canada 57 (ACA57) baada ya kuwasilisha pasipoti yake ya
Canada.
Wakili huyo alikuwa amesema
hakuwa na pasipoti hiyo alipowasili uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, Nairobi
Jumatatu wiki iliyopita.
Wakili wake Cliff Ombeta
hata hivyo ameambia BBC kwamba mteja wake hakuwa na pasipoti hiyo.
Aidha, amesema kwa sasa
hawezi kuthibitisha iwapo Bw Miguna yumo safarini kuelekea Canada.
Safari ya ndege kutoka Dubai
kwenda Toronto huchukua takriban saa 13.
Bw Miguna ndiye
aliyeidhinisha kiapo cha Bw Raila Odinga alipokuwa anajiapisha kuwa 'Rais wa
Wananchi' mwezi Januari.
Bw Miguna Miguna alijaribu
kurejea Kenya Jumatatu lakini akazuiwa kuingia baada yake kudaiwa kutowasilisha
pasipoti ya Canada ambayo ilitumiwa kumsafirisha kwa nguvu hadi Canada.
Wakili huyo alisisitiza
kwamba ni raia wa Kenya na hafai kuzuiwa kurejea.
Taarifa zinasema Bw Miguna,
ambaye pasipoti yake ya Kenya ilitwaliwa na polisi kabla ya kuondolewa kwake
Kenya mwezi jana, alikuwa ametakiwa kuwasilisha ombi la kupata visa ya kukaa Kenya
kwa miezi sita kwa kutumia pasipoti hiyo yake ya Canada.
Alikataa jaribio hilo na
badala yake kutoa kitambulisho chake cha taifa kuonesha kwamba yeye ni Mkenya
na kutaka aruhusiwe kuingia.
Bw Miguna, aliyekuwa
amewasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mwendo wa saa nane
adhuhuri, alikesha kwenye uwanja huo.
Maafisa walijaribu
kumsafirisha kutoka uwanja huo mara ya kwanza kwa kutumia ndege ya shirika la
Emirates ambayo ilikuwa inaelekea Canada kupitia Dubai usiku huo wa Jumatatu
lakini hawakufanikiwa.
Hata hivyo,
walifanikiwa usiku wa kuamkia Jumatano.
Bw Miguna asubuhi aliandika
kwenye Facebook kwamba aliamka na kujipata yuko Dubai na kwamba anahitaji
matibabu.
Mwanasiasa huyo alisema
alisindikizwa na afisa wa idara ya ujasusi na kwamba amemuona daktari uwanja wa
ndege.
Bw Miguna alisisitiza kwamba
hatasafiri kwenda popote ila kurejea Nairobi.
Serikali imechukua hatua hiyo
licha ya kuwepo kwa maagizo ya mahakama ya kuzuia kutimuliwa kwake na ya
kuitaka serikali kufanikisha kurejea kwake nchini humo.
Jaji wa Mahakama Kuu George
Odunga aliwapata na hatia waziri wa usalama nchini humo, mkuu wa polisi na mkuu
wa idara ya uhamiaji ya kukaidi maagizo ya mahakama iwapo wangekataa
kumwachilia huru.
Aliwatoza faini ya Sh200,000
(Dola 2,000) kila mmoja.
No comments:
Post a Comment