The Look Company Limited yaendesha semina kwa mawakala wa Miss Tanzania...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KAMPUNI ya The Look Company Limited imeendesha semina kwa mawakala wa Miss Tanzania nchini ikiwa ni mchakato wa kuanza kwa shindano hilo kwa mwaka wa 2018.

Mkurugenzi wa The Look Company Limited Basilla Mwanukuzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mawakala wa shindano la Miss Tanzania jijini Dar es Salaam.

Semina hiyo imekuja siku chache baada ya uzinduzi wa shindano la Miss Tanzania kwa mwaka hu, uliofanywa na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe ambalo litasimamiwa na kampuni hiyo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam  wakati wa ufunguzi wa semina Mkurugenzi wa kampuni hiyo ambaye pia ni mwandaaji wa shindano hilo aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1998 Basilla Mwanukuzi, amesema lengo ni kuwaelimisha mawakala hao.

“Siku  ya leo tumefungua semina ya mawakala, mawakala wetu nchi nzima ambao wao ndiyo watakaoenda kuandaa mashindano ya mikoa na kanda,” amesema Mwanukuzi.

“Nia na madhumuni ya semina hii ni kuwaelimisha, kwa sababu wapo ambao ni wapya, hasa kuwaelimisha kuhusiana na mashindamo mazima ya Miss Tanzania, lakini pia wabebe maono ya The Look Company Limited ambayo iko nayo kwa sasa ili waweze kuongea lugha moja,” ameongeza.

Ameongeza kuwa semina hiyo itasaidia mawakala hao watakapokwenda kutafuta  warembo mikoani na kwenye kanda watulete warembo ambao haswa watanzania wanatarajia wawe wawakilishi wao katika mashindano ya dunia.

“Tukumbuke kwamba mashindano ya fainali yanapokea washindi wa kutoka kwenye mikoa na kanda, kwa hiyo ni vyema kuwaelimisha, kuwasihii na kuwaongoza  matarajio kitu gani tunategemea, wao ndiyo hasa wanaenda kutafuta Miss World,” amesema.

Mkurugenzi huyo amsema pia ilikuwa ni kuwaelimisha waweze kufanya kazi yao  kulingana na tamaduni, sheria, taratibu za nchi na za kampuni amabyo ndiyo waandaaji.
Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza akizungumza alipokuwa akifungua semina ya mwawakala wa shindano la Miss Tanzania Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa nchini (BASATA) Godfrey Mngereza amewataka mawakala hao kuhakikisha wanasimamia shindano katika ngazi ya mkoa na kanda  kwa haki ili kupata mrembo atakaeweza kufanya vizuri katika shindano la dunia.
Miss Tanzania 2010 na wakala Genevieve Mpangala akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa semina hiyo jijini Dar es Salaam.

Naye Miss Tanzania wa 2010 Genevieve Mpangala ambaye pia ni wakala amewataka warembo kujitokeza katika shindano hilo kwa mwaka huu ili kuweza kuwania nafasi ya kuiwakisha nchi katika ngazi ya dunia.

 
Sehemu ya mawakala waliohudhuria semina hiyo



Mkurugenzi wa The Look Company Limited Basilla Manukuzi akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa semina hiyo jijini Dar es Salaam.


Ofisa kutoka BASATA akitoa semina kwa mawakala wa Miss Tanzania waliohudhuria jijini Dar es Salaam.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search