Uhamiaji watoa ufafanuzi sakata la Nondo...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
IDARA ya
Uhamiaji imesema Watanzania wote waliozaliwa kuanzia mwaka 1978 wanapaswa kuwa
na cheti cha kuzaliwa.
Ofisa Uhamiaji Mkoa wa
Dar es Salaam, Crispin Ngonyani amesema hayo leo Jumatatu Aprili 9, 2018
alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Ngonyani amesema hayo
alipotoa ufafanuzi kuhusu maagizo yaliyotolewa na Uhamiaji kwa mwanafunzi wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Abdul Nondo ya kuwasilisha vyeti vya
kuzaliwa vya wazazi wake, babu na bibi zake linavyoweza kutekelezwa.
"Tulimweleza Nondo
na mwanasheria wake kuwa, kama hawana vyeti vya kuzaliwa wanaweza kuleta
affidavit (hati ya kiapo) na hilo tulikubaliana," amesema Ngonyani.
Amesema, "Lakini
kama mtu umezaliwa kuanzia mwaka 1978 kwa sheria yetu lazima uwe na cheti cha
kuzaliwa na tukikuomba utapaswa kutuonyesha kwa hiyo wananchi wanapaswa kulijua
hili."
Nondo ambaye ni
mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) alihojiwa Aprili 5, 2018
kuhusu uraia wake na ametakiwa kupeleka vielelezo kuthibitisha uraia wake
vikiwamo vyeti vya wazazi, bibi na babu wa pande zote
No comments:
Post a Comment