Yanga yavutwa shati na Singida United...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
LIGI kuu soka Tanzania Bara imeendelea tena hii leo kwa michezo kadhaa kupigwa kwenye viwanja mbalimbali huku bingwa mtetezi klabu ya Yanga SC ikilazimishwa sare ya bao 1- 1 dhidi ya Singida United uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Bao la Singida United likifungwa na Papy Kambale dakika ya pili ya mchezo huo wakati Yanga SC ikisawazisha kupitia kwa Abdalla Shaibu kunako dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza.
Yanga SC na Singi United hazijawahi kufungana ndani ya dakika 90 toka kukutana kwao wakati kwenye michezo mingine dimba la Mwadui Complex mjini Shinyanga. Mwadui FC 2-1 Lipuli FC, Mbao FC 2 – 1 Njombe Mji, Standa United 1 – 3 Maji Maji,
Simba SC kesho itashuka dimbani kuikabili Mbeya City wakati Yanga SC wakisafiri kwenda kucheza mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi Welayta Dicha.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search