Jaffo: Wazazi hakikisheni vijana wanu wanapata elimu ya Dini ili wawe na maadili...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
WAZIRI Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Seleman Jaffo amewataka wazazi kuhakikisha vijana wao wanapata elimu ya Dini itakayowasaidia kukua na kuishi katika maadili.

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika Fainali ya Mashindano ya kuhifadhi Qur’an Tukufu ya Afrika Mashariki inayoandaliwa na Taasisi Almanahilul Irfan Islamic Centre.

“Niwasishii wazazi waendelee kuwapatia elimu ya dini vijana ili kupata maadili yatakayowaongoza, kila mtu ahakikishe na atambue kuwa ni wajibu wake kuhakikisha kijana wake anakuwa na maadili,” amesema Jaffo.

Amesena kama  watalelewa katika maadili hawataweza kushawishiwa kuvuruga amana ya nchi na badala yake watawajibika kuilinda na aliwapongeza wazaizi kwa kuwawizesha vijana kujifunza Qur’an.

Kwa Upande wake Makamu wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dk. Mohamed Gharib Bilal, amewataka viongozi wa Dini kuendelea kuhamasisha vijana kusoma Qur’an.
Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam Alhad Mussa amesema lengo la kuhifadhisha Qur’an kwa vijana ni kutaka kuwafanya waishi kwa kuakisi tabia ya Qur’an kama ilivyokuwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w).

“Hii inasaidia kutengeneza vijana wenye maadili na wasio sumbua nchi, kijana anayehifadhi Qur’an atakuwa ni kijana mwenye madili na kioo,” amesema Sheikh Mussa.

Amesema mwaka ujao shindano hilo litaanzia katika nganzi ya kitaifa, Afrika Mashariki, Afrika na katika ngazi ya kimataifa.

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, Ayoub Mohammed  Mahmoud amesema shindano hilo linalenga kuendeleza Uislamu na umoja na aliwataka vijana wote walioshiriki katika shindano kuyatumia vizuri mafunzo waliyopata.

Aidha aliomba shindano hilo kutumika katika kuimarisha muungano. Lakini pia aliwataka wananchi wasio waislamu kwa kipindi hiki cha mfungo wa ramadhan  kuwa na subra ili kulinda amani.

Naye mlezi wa taasisi hiyo aliyekuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa akitoa shukurani ametoa wito kwa taasisi nyingine kujitokeza katika kusaidia mashindano kama hayo.

Kwa upande wa shindano, lilikuwa na makundi manne ambayo ni ya Juzuu 10, Juzuu 20, Juzuu 3 na Juzuu 30 ambapo mshindi wa kwanza ni Abubakar Mohammed Omar-Tanzania Bara, wapili ni Amanya Adilu Ally-Uganda na watatu ni Suleman Ally Matano-Kenya.












About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search