Banki ya DCB yatoa mikopo ya bilioni 9.2 kwa wajasiriamali Ilala...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

BANKI ya DCB imesema toka walivyoingia katika makubaliano ya kutoa mikopo na Manispaa ya Wilaya ya Ilala mwaka 2014 kwa wanawake na vijana wajasiriamali  tayari wameshaweza kutoa mikopo ya takribani  bilioni 9.2  kwa vikundi 2978.


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB Godfrey Ndalahwa(kulia) katika banda la benki hiyo wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya siku mbili ya wajasiriamali wa Wilaya ya Ilala yanayofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.



Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Godfrey Ndalahwa alipokuwa akizungumza  wakati wa maonyesho ya bidhaa za wajasiriamali yaliyofunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.

 “Changamoto iliyopo  kwa sasa ni uhitaji wa fedha kwani wanawake na vijana wanaohitaji mikopo hiyo ni wengi katika manispaa na kuiomba Halmashauri kuongeza fedha za mfuko huo ili kuwezesha benki kuwahudumia wajasiriamali wengi zaidi.

“Tumelisikia ombi la wajasiriamali la kutaka kuboreshwa kwa mikopo ikiwemo kuongezwa kwa kiasi cha fedha pamoja na kukopesha vitendea kazi na vifaa kazi, sisi kama DCB benki mteja wetu atakapohitaji vifaa atakuja kwetu na tutakaa chini na kuingia makubaliano,”amesema na kuongeza Ndalahwa.

Katika kuelekea kwenye uchumi wa viwanda kama ilivyo adhima ya serikali ya  awamu ya tano, Ndalahwa amewashauri wanawake na vijana kuzingatia ubunifu na kutumia fursa za kiuchumi kupata mitaji na kujiendeleza  na kwamba  benki itandelea kutoa fursa za mitaji kwa wajasiriamali wa aina hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza  baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya wajasiriamali hao na kujionea namna wanavyofanya kazi  zao amesema wameonesha kuwa mikpo waloyokuwa wanaipata imekuwa na msaada mkubwa sana kwao na wameweza kujiendeleza katika kukuza mitaji ya biashara zao na hata wengine waliweza kuanzisha biashara nyingine na kujipatia faida.

“Wajasiriamali hawa wameonekana kufikia malengo yaliyowekwa na rais John Magufuli kwa kuanzisha viwanda, tumeona jinsi gani wameweza kutumia nafasi walizozipata hususani katika mikopo waliyoipata na kujiendeleza zaidi,”amesema Mjema.

Benki ya DCB  kwa sasa hapa nchini inasifika kwa kuwa  mstari wa mbele katika utoaji wa mikopo kwa vikundi mbalimbali vinavyojishugulisha na utengenezaji wa bidhaa za vyakula, nguo, viatu na hata dawa za kusafishia ndani na vyooni.

Habari katika picha.











About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search