BREAKING NEWS!! 'KIMBEMBE CHA RUZUKU CUF' MAALIM AIBUKA KIDEDEA !!
Maalim Seif Sharrif Hamad |
Amri hiyo ya Mahakama Kuu imekuja baada ya Jopo la Mawakili
wasomi wa Chama wanaoiwakilisha Bodi ya Wadhamini ya CUF (THE REGISTERED
TRUSTEES OF THE CIVIC UNITED FRON (CUF-CHAMA CHA WANANCHI) Mhe. Juma Nassor,
Mhe Daimu Halfani na Hashim Mziray kuwasilisha maombi hayo mbele ya Mahakama
Kuu kuiomba Mahakama Kuu kutoa Amri hiyo kwa kuwa fedha zilizotolewa awali
Milioni 369 hazijulikani zimetumika vipi, na hazikuwa katika mikono salama wala
hakuna udhibiti wowote wa Chama –CUF juu ya fedha hizo ikizingatiwa kuwa
Lipumba alishavuliwa Uanachama. Wakili Msomi Juma Nassor aliyewasilisha maombi
hayo aliweka mkazo na kusisitiza kuwa kwa mazingira yaliyopo ni vyema na Busara
kwa fedha za umma zilizopaswa kutolewa kama Ruzuku kwa Chama Cha CUF kwa sasa
ZIENDELEE KUBAKIA SERIKALINI. Aidha, Mawakili wasomi wameiomba Mahakama Kuu
amri hiyo pia ifungamane na Kesi ya Msingi namba 23/2016 ya kuhoji maamuzi ya
Msajili kumtambua Lipumba kwa Nafasi ya Uenyekiti iliyopo mbele ya Jaji Kihijo
ambayo kwa sasa imekatiwa Rufaa/maombi ya kufanyiwa Marejeo-REVISION mbele ya
Mahakama ya Rufaa-Tanzania.
Mhe Jaji Dyansobela amekubaliana na Hoja zote hizo
zilizowasilishwa kwa HATI YA DHARURA.
No comments:
Post a Comment