MAKONDA NDANI YA KAMATI YA BUNGE

RC MAKONDA AWASILI DODOMA, KUHOJIWA NA KAMATI YA BUNGE LEO!

WhatsApp Image 2017-03-29 at 12.40.19 PMMkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewasili bungeni mjini Dodoma leo asubuhi na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Bunge ikiwa ni kuitikia wito wa Bunge wa kumtaka kufika mbele ya kamati.
RC Makonda amepokelewa na Owen Mwandumbya ambapo aliitwa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge akitakiwa kujieleza kuhusu kauli aliyoitoa inayodaiwa kuwa ni ya kulidharau na kulikashifu kwa wabunge.
WhatsApp Image 2017-03-29 at 12.40.20 PM
Akitoa hoja katika mkutano wa bunge uliopita, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara alisema kuwa viongozi mbalimbali hasa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wamekuwa wakitumia madaraka yao vibaya kiasi cha kuingilia majukumu yasiyo yao, na wakati mwingine kuingilia majukumu ya Bunge, na kutolea mfano Paul Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Alexander Mnyeti.
==========================================================
Hapa chini ni picha za RC Makonda akihojiwa na kamati ya bunge leo mjini Dodoma.
WhatsApp Image 2017-03-29 at 1.45.42 PMWhatsApp Image 2017-03-29 at 1.45.42 PM (1)

Source: www.swahilitimes.com

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search