CCM YATAJA WAGOMBEA WAKE 'EALA'

·       12 KUOMBA RIDHAA UBUNGE AFRIKA MASHARIKI KUPITIA CCM
·       TUMEZINGATIA 'GENDER' NA UWIANO WA MUUNGANO

Majina ya walioteuliwa kugombea.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeteua wanachama 12 ambao watakwenda Bungeni kuomba ridhaa ya kuiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (Eala).

Majina yaliyotajwa yamezingatia uwakilishi wa pande zote za muungano, uwiano wa wanawake na wanaume pamoja na uadilifu wa wanachama wenyewe.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema chama chake kina nafasi sita za uwakilishi lakini wameamua kutoa watu 12 ili kuwapa nafasi kubwa Wabunge kuchagua wanaofaa zaidi.

Walioteuliwa na CCM kutoka bara upande wa wanawake ni Zainabu Kawawa, Happiness Lugiko, Francy Nkuhi na Happiness Mgalula.

Wanaume kutoka bara ni Dk Ngwaru Maghembe, Adam Kimbisa, Anamringi Macha na Charles Makongoro Nyerere.

Kwa upande wa Zanzibar wanawake ni Maryam Ussi Yahya na Rabia Abdallah Hamid. Wanaume ni Abdallah Hasnu Makame na Mohammed Yussuf Nuh.

Source: CCM - Itikadi na Uenezi 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search