#HABARI KAMILI: YALIYOJIRI KATIKA UZINDUZI WA TAARIFA YA UHAKIKI WA VYETI KWA WATUMISHI UMMA MJINI DODOMA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli akiionyesha Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma kwa wananchi waliohudh,.uria uzinduzi wa Taarifa hiyo katika ukumbi wa Chimwaga Mjini Dodoma,Kushoto kwake ni Makamu wa Rais Mhe.Samia Hassan Suluhu na Kulia kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM)Prof.Idris Kikula.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu wakifwatilia Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma mara baada ya kuizindua katika Viwanja vya Chimwaga Mjini Dodoma leo.Kushoto kwa Makamu wa Rais ni Waziri nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.George Simbachawene.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli ,Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu na Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa wakibonyeza kitufe kuzindua wiki ya Maandimisho ya Miaka 10 ya Chuo kikuu cha Dodoma(UDOM).

Wananchi mbalimbali wakifuatilia Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli wakati akipokea Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma katika viwanja vya Chimwaga Mjini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli akihutubia wananchi katika Ukumbi wa Chimwaga Mjini Dodoma leo kabla ya kupokea Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma.

Waziri Mkuu Mhe.Kassima Majaliwa akitoa salamu kwa wananchi waliofika katika ukumbi wa Chimwaga leo Mjini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma kutoka kwa Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe.Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga,Mjini Dodoma.

Viongozi mbalimbali waliohudhuria Hafla hiyo wakiwa katika ukumbi wa Chimwaga wakisubiri upokeaji wa Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma leo Mjini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Makamu wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM)Prof.Idris Kikula kabla hajapokea Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma.

Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu akizungumza katika hafla ya upokeaji wa Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma Mjini Dodoma leo.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai,Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa na Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof,Joyce Ndalichako wakifuatilia hotuba ya Rais wa jahuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa upokeaji wa Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma Mjini Dodoma leo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli, akikata utepe kuzingua Taarifa ya Uhakiki wa Vyeti kwa watumishi wa Umma Mjini Dodoma leo.Wengine pichani Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe.Angela Kairuki na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM)Prof.Idris Kikula.
Picha zote na Daudi Manongi-MAELEZO,DODOMA
No comments:
Post a Comment