#Marekani yajishusha; yesema iko tayari kwa mazungumzo na Korea Kaskazini !
![]() |
Rex Tillerson (kulia) na balozi wa Marekani kwenye UN Nikki Haley |
Marekani
iko tayari kwa mazungumzo na Korea Kaskazini yenye lengo la kuondoa zana za
nuklia kutoka eneo hilo, kwa mjibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa
Marekani Rex Tillerson.
Lakini
amesema kuwa Marekani itatumia nguvu za kijeshi ikiwa itahitajika.
Waziri
wa mashauri ya nchi za kigeni wa China, mshirika mkubwa wa Korea Kaskazini,
anasema makubaliano ya amani ndio njia pekee.
Bwana
Tillerson aliliambia baraza la ulinza la Umoja wa Mataifa kuwa tisho la Korea
Kaskazini la kushambulia majirani zake na zana za nuklia.
Maelfu
ya wanajeshi wa Marekani wako nchi majirani wa Korea Kaskazini ikiwemo Korea
Kusini na Japan.
Tillerson
amezitaka nchi wachama wa Umoja wa Mataifa kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo na
kupunguza uhusiano wao wa kidiplomasia na nchi hiyo.
"Kwa
miaka kadha Korea Kaskazini imekuwa ikiendesha kwa nguvu mpango huu
hatari."
"Ni
wakati wetu kuchukua hatua na kudhibiti hali," Tisho la Korea Kaskazini la
kufanya shambulizi la nuklia dhidi ya Korea Kusini au Japan ni la kuwezekana,
na ni muda tu kabla ya Korea Kaskazini kufanikiwa kupata uwezo wa kushambulia
Marekani." alisema Tillerson.
No comments:
Post a Comment