MAONI YA WATU MBALIMBALI KUHUSU RAIS MAGUFULI KUMTEUA PROF. KITILA MKUMBO

Kitila-MkumboRais Dkt John Pombe Magufuli leo Aprili 4, 2017 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali kutokana na baadhi ya viongozi waliokuwepo kustaafu, kutenguliwa au kuhamishwa.
Rais Dkt Magufuli ameteua viongozi mbalimbali kuwa makatibu wakuu lakini miongoni mwao, mmoja tu ndiye aliyezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii.
Rais Magufuli amemteua Prof. Kitila Alexander Mkumbo ambaye ni mwanachama wa ACT- Wazalendo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Prof. Kitila Alexander Mkumbo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anachukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu.
Sababu kuu mbili zilizosababisha watu kujadili zaidi uteuzi huu ni, moja, kauli ambayo Prof. Mkumbo aliyoitoa kipindi cha nyuma kuhusu wahadhiri kuteuliwa kutoka vyuoni ambapo alisema, “Huu utaratibu wa kuwateua wasomi tu ambao ni walimu na wanataaluma kutoka vyuo vikuu hasa Chuo kikuu cha Dar es salaam si mzuri maana rais haoneshi kuwaandaa wengine kuchukua nafasi zao, tuachwe wasomi tufanye kazi za kitafiti na kitaaluma.”
Wengi wamehoji je atasimamia kauli yake? Lakini pili ni kauli ya Rais Magufuli aliyoitoa kwenye mkutano wa hadhara akiwa Unguja kuwa kwenye serikali yake hatoteua mtu kutoka chama cha upinzani.

Source:Swahili times

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search