SIMU ZA KISASA (SMARTPHONES) ZINAVYOWEZA KUTUMIKA KUPIMA NGUVU ZA KUIUME

sperm_640

Watafiti wa Marekani wamegundua kifaa kipya cha ‘smartphone’ kilicho na uwezo wa kupima na kubaini kama mbegu za uzazi za mwanaume zina uwezo wa kumfanya mwanamke kuwa mjamzito.
Kutokuwa na uwezo wa kuzaa kumewaathiri watu zaidi ya milioni 45 duniani. Zaidi ya 40% ya matatizo ya uzazi yanasababishwa na kiwango hafifu cha mbegu za kiume.
Teknolojia iliyochambuliwa katika makala ya ‘Science Translation medicine’ imelenga kuleta urahisi kwa wanaume kujipima wenyewe uwezo wa mbegu zao za uzazi.
“Tumetaka kuleta utatuzi na kufanya upimaji wa uwezo wa mbegu za kiume kuwa rahisi na unaopatikana kama vile vipimo vya ujauzito vya wanawake” alisema Hadi shafee daktari katika kitengo cha uhandisi wa madawa katika hospitali ya Wanawake Brigham.
“Wanaume hutakiwa kuleta manii katika hospitali hali ambayo huwafanya kuwa na woga  na kuudhika”
Kipimo hiki kipya, kinaweza kutoa majibu ya manii ndani ya muda wa dakika 5.
Kipimo hichi kinafanya kazi kupitia muunganiko wa ‘smatphone’ na chombo cha kuwekea manii, ilieleza ripoti hiyo.
Watafiti hao, walikifanyia majaribio kipimo hicho kwa kutumia manii za wanaume 350 katika kituo cha ‘Massachusetts General Hospital fertility Centre’.
Kifaa hicho kilitoa majibu yenye ukweli kwa asilimia 98. Gharama ya kifaa hicho ni dola za kimarekani 4.45 sawa na shilingi za kitanzania 10000 tu.
Waliongeza kuwa uwepo wa kifaa hicho utarahisisha ufuatiliaji wa afya za uzazi kwa watu binafsi pasipokuwa na haja ya kwenda hospitali.
Aidha kifaa hicho bado kipo katika hatua za mwisho za majaribio na kitazinduliwa rasmi kwa matumizi baada ya kukaguliwa na kitengo cha ‘US Food and Drug Administrational Approval’ chenye mamlaka ya kuthibitisha kama kifaa hicho kinafaa kwa matumizi.
Source Swahil times

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search