MORINHO ATOBOA SIRI: CHRIS SMALLING NA PHIL JONES WATASUBIRI KWANZA


Phil Jones na Chris Smalling
Phil Jones (pili kushoto) anaonekana kuumia baada ya kukabiliwa na Chris Smalling (kati) wakati wa mazoezi
Mabeki wa Manchester United Chris Smalling na Phil Jones walipata majeraha ya kuwaweka nje kwa muda mrefu walipokuwa wanachezea timu ya taifa ya England, meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho amesema.
Jones, 25, aliumia kwenye kidole wakati wa mazoezi akikabana na mpinzani.
Taarifa zinasema kisa hicho kilimhusisha Smalling.
Beki mwenzake Smalling, 27, alipigwa picha akiwa amefungwa kitambaa mguuni baada ya kuumia pia wakati wa mazoezi.
Nahodha wa United Wayne Rooney hata hivyo amepata nafuuu na atarejea kuwachezea dhidi ya West Brom Jumamosi baada ya kupona jeraha la goti.
Rooney, 31, alikosa mechi United za karibuni zaidi walizocheza United.
Kutokana na kuumia kwa Smalling na Jones, Mourinho amemwita beki wa miaka 19 Axel Tuanzebe kikosini kwa ajili ya mechi hiyo.
Tuanzebe amechezea United mechi moja pekee ya ushindani, mechi ambayo walilaza Wigan 4-0 katika Kombe la FA Januari.
United watakuwa pia bila mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic na kiungo wa kati Ander Herrera wanaoumikia marufuku.
Pia, watamkosa Paul Pogba, anayeuguza jeraha la misuli ya paja.

Source: Swahili BBC London

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search