NAY WA MITEGO - LIVE COVERAGE XXL YA CLOUDS FM

  1. 'Mimi sina ugomvi na serikali, mimi ni mwanamuziki na sipendi kubishana na Serikali'-Nay wa Mitego
  2. 'Nilikamatwa lakini nilikuwa na amani kabisa, na niliongea na mama yangu nikamwambia awe na amani'-Nay wa Mitego
  3. 'Sitaki kuwalaumu polisi jinsi walivyokuja kunikamata kwa sababu wao wanatumwa'-Nay wa Mitego
  4. 'Niliambiwa nimefunguliwa kesi, nikaambiwa ni kesi ya matusi'-Nay wa Mitego

Mwanamuziki Emmanuel Elibariki maarufu Nay wa Mitego amesema kuwa usalama wa maisha yake kwa sasa ni mdogo sana kutokana na baadhi ya watu kumtisha kutaka kumuua.
2Nay wa Mitego ambaye siku za hivi karibuni alikuwa matatizoni kutokana na wimbo wake wa WAPO ameandika kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa yeye ni msanii na anachofanya ni muziki si mambo mengine hivyo hawezi kutishika.
Aidha, Nay amesema kuwa licha ya kuwa anakumbana na vitisho vyote hivyo hawezi kuhama nchi wala kukimbilia popote na kwamba ataifia hapa hapa nchini;
“Usalama wa Maisha yangu umekua Mdogo kwasasa, Wana panga kunipoteza ikibidi nisiwepo kabisa kwenye hii Dunia. Nipo tayari kwa chochote wanacho panga kufanya Coz sijajipanga kupambana nao, Mimi ni Mwana Muziki si vingine. Kwa chochote kitachotokea Familia yangu itakua na chakuongea,” aliandika Nay.
Aliandika pia, “Siwezi kuhama Nchi wala kukimbia nitafia hapa hapa. Na siko tayari kupindisha Chochote.! Nyie Ndo mtanilinda. Sina Mlinzi na sitarajii kua na mlinzi. OnlyGod🙏🏿#Wapo #Truth.”


Source: swahilitimes.com

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search