SALUM MKEMI NAE YAMKUTA YA HAJI MANARA, BODI YA LIGI TANZANIA YAMSHITAKI KWENYE KAMATI YA NIDHAMU



Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Salum Mkemi amefunguliwa na mashitaka na Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB).


TPLB inamtuhumu Mkemi kutoa matamshi ya kuudhi dhidi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mkemi anadaiwa kuwadhalilisha viongozi wa TFF kwa madai kwamba alidai amefikisha suala la viongozi wa kamati ya Saa 72 Takukuru.
Hata hivyo, TFF na bodi ya ligi ziliendelea kukaa kimya bila ya kuchukua hatua hadi wadau walipoanza kulalamika kuhusiana na kufungiwa kwa Msemaji wa Simba, Haji Manara.
Baada ya hapo, inaonekana ndiyo TFF imekurupuka sasa ikitaka kuona Mkemi naye anachukuliwa natua “ikizuga” kupitia bosi ya ligi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search