Aliembusu Nyoka Yamemkuta haya !

Mwanamume mmoja katika jimbo la Florida nchini Marekani ambaye alijaribu kumbusu nyoka na badala yake nyoka huyo akamuuma, anaendelea kupata matibabu hospitalini.
Nyoka huyo alipatwa na Charles Goff, mkaazi wa kaunti ya Putnam kaskazini mwa jimbo la Florida siku ya Jumatatu.
Siku moja baadaye jirani wake ambaye alitajwa na kituo cha CBS kama Ron Reinold alianza kucheza nyuko huyo kwa kujaribu kumbusu.
Bwana Reinold alisafirishwa kwa njia ya ndege na kwa sasa anaendelea kupata nafuu hospitalini,.
Kijana mmoja alisema, "nitambusu mdomoni," ndipo nyoka huyo akamuuma usoni, bwana Goff alililiambia shirika la habari la Action News Jax.
Kituo cha First Coast News kilisema kuwa muathiriwa alikuwa na fahamu lakini katika hali mbaya. Nyoka huyo anaaminika kutokeka baada ya kisa hicho.
Haijulikani sababu iliyochangia bwana Reinold ajaribu kumbusu nyoka huyo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search