BREAKING NEWS!! Philemon Ndesamburo aaga Dunia, #SHARE ..Mwanawe Mhe. Lucy Owenya akubwa na Taharuki !

Tumepokea habari ya kusikitisha ya kifo cha ghafla cha Mwanansiasa Mkongwe hususan kwenye Anga za Siasa za Upinzani Nchini' Bwana Philemon Ndesamburo.


Mtoto wa Marehemu Mbunge wa Viti Maalum Maalum Mkoa Kilimanjaro Mhe. Lucy Owenya(Pichani chini), aliekuwa Bungeni Mjini Dodoma akihudhuria vikao vya Bunge la Bajeti, alikumbwa na mshtuko mkubwa baada ya kupokea Taarifa hizo.


Kwa mujibu ya maelezo yanayotembea mtandaoni na ambayo Matukio Blog inayafanyia kazi, Mzee Ndesamburo amefariki mara baada ya kufikishwa hospitalini kufuatia kupoteza nguvu ghafla alipokuwa 'akisaini cheki' kwa ajili ya mchango wa Rambirambi kwa wafiwa waliopoteza wapendwa wao kwenye ajali ya basi la wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent.

Mzee Ndesa au 'Ndesa Pesa' kama mashabiki wake walivyopenda kumuita, alizaliwa Mwaka 1935, na amewatumikia wananchi wa Moshi Mjini kwa kuanzia mwaka 2000 mpaka alipoamua kustaafu rasmi nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo kwa tiketi ya CHADEMA.


#Matukio Blog inaungana kuwapa pole wafiwa na kumuombea Marehemu Ndesamburo !

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search