DSE: Mauzo soka la hisa yapungua...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Salha Mohamed 

Na Salha Mohamed, Dar es salaam

THAMANI ya mauzo ya soko la hisa (DSE),  imepungua kutoka  bilioni 4 Novemba  30, 2017  hadi  bilioni 3.7 Desemba 8, 2017.


Mary Kinabo

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Ofisa Mwandamizi wa Masoko, Mary Kinabo amesema mbali na kupungua kwa mauzo, idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepanda. 

"Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepanda kutoka hisa milioni 7.6 ya wiki iliyoisha Novemba 30/2017  hadi hisa milioni 8 ya wiki inayoishia Desemba 8/2017",amesema.

Amesema ukubwa wa mtaji wa kampuni zote zilizoorodheshwa katika soko umepungua kwa shilingi bilioni 433 kutoka shilingi trilioni 21 wiki iliyopita hadi shilingi trilioni 20.8 wiki iliyoishia Desemba 8/2017.

Amefafanua kuwa punguzo hilo ni kutokana a kushuka kwa bei za Uchumi Supermarket Ltd(USL)  kwa asilimia 10,Acacia Mining (ACA) kwa asilimia 10,Kenya Commercial Bank(KCB) kwa asilimia 5 na DCB kwa asilimia 1.

Amesema ukubwa wa mtaji katika Kampuni za ndani umepanda kwa shilingi bilioni 88 kutoka trilioni 10.035 hadi kufikia shilingi trilioni 10.13 wiki hii kutokana na kupanda kwa bei ya hisa za kampuni ya bia TBA kwa asilimia 2.

Amesema kiashiria cha kampuni zilizoorodheshwa katika soko (DSEI)  kimepungua kwa point 45 kutoka point 2,207 hadi point 2,162 kutokana na kushuka kwa bei ya hisa za Uchumi Supermarket Ltd (USL), Acacia Mining (ACA), Kenya Commercial Bank (KCB). 

"Kiashiria cha sekta ya Viwanda kimepanda kwa point 78 kutoka pointi 5,293 hadi pointi 5,372,"amesema.

Amesema mauzo ya hati fungani katika wiki inayoishia Desemba 8/2017 yalikuwa shilingi bilioni 1.4 kutoka shilingi milioni 17 wiki iliyopita Novemba 30/2017.

"Mauzo haya yalitokana na hatifungani 5 za serikali zenye jumla ya thamani ya shilingi bilioni 1.6 kwa jumla ya gharama ya shilingi bilioni 4,"amesema. 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search