Exclusive News! Trump asalimu amri, sasa yuko Tayari kukutana na hasimu wake mkuu kiongozi wa korea Kaskazini.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kukutana uso kwa uso na rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un endapo atapata nafasi ya kufanya hivyo.
Akijibu
swali katika mahojiano maalum na jarida maarufu la Bloomberg jana tarehe 1 May,
Trump alisisiza bado ni ndoto yake kubwa kukutana na kiongozi huyo mtata wa N.
Korea.. “Kweli nisingesita kufanya hivyo, tena hilo ni jambo la heshima kubwa
kwangu”
Kauli hiyo
ya Trump imeonekana kama hatua ya ‘kulamba matapishi yake’ imekuja wakati hali
ya sintofahamu ikizidi kutamalaki kufuatia Marekani na washirika wake kujiandaa
kufanya majaribio kadhaa ya silaha za kiatomiki kujibu majaribio kama hayo
yaliyofanywa na Pyongyang.



No comments:
Post a Comment