Kutoka Bungeni: Ona hapa Wabunge walivyopaza sauti kumnasua Halima Mdee kifungoni !

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenister Mhagama amependekeza kufanyika kwa mabadiliko ya hoja na kupendekeza Mhe. Mdee asamehewe... hata hivyo ametoa tahadhari endapo atatenda kosa jengine la kudharau mamlaka ya Bunge utekelezaji wa adhabu uanze mara moja bila kuitisha kikao cha kamati ya maadili.

Kupitia vikao vya Bunge la Bajeti linaloendelea Makao Makuu Dodoma, leo Jumanne Wabunge wa pande zote bila kujali itikadi za vyama vyao, wamemwomba Spika kutoa msamaha kwa Mbunge Halima Mdee aliyepewa adhabu ya kutohudhuria vikao vya Bunge la Bajeti vilivyobakia.

Baada ya Wabunge kwa umoja wao kuomba kiti cha Spika kutompa adhabu hiyo Halima Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA, Bunge limetangaza kumsamehe na ataendelea na vikao kwa sharti la kutorudia tena kosa. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search