Mwanamama wa uzito mkubwa 'asababisha mzozo' hospitalini !

Mwanamke aliyekuwa na uzani mzito zaidi duniani atasafirishwa hadi katika milki za kiarabu UAE baada ya mzozo kuhusu uzani wake katika hospitali ya India ambapo alikuwa akipatiwa matibabu.
Hospitali ya Saifee mjini Mumbai ilisema kuwa Eman Abd El Aty alifanyiwa upasuaji wa kupunguza uzani na sasa alikuwa huru kuondoka kwa sababu ana uzani wa kilo 172 kutoka kilo 500 alizokuwa nazo awali.
Lakini dadake alimshutumu daktari wa upasuaji huo kwa kudanganya na kumuomba amruhusu dadake aendelee kukaa katika hospitali hiyo.
Kwa sasa ataelekea katika hospitali ya Burjeel huko Abu Dhabi.
Taarifa iliotolewa na daktari wa bi Abd El Aty imesema kuwa atapatiwa matibabu muhimu kwa kuwa hospitali hiyo iko karibu na nyumbani.
Hospitali ya Saifee imeongezea kwamba ilikuwa fahari kwa juhudi zilizofanywa na kundi la madaktari wake ikidai kuwa mgonjwa huyo aliwasili kupitia ndege ya kubebea mizigo na sasa anarudi kama abiri katika ndege ya watu.
Mapema hospitali hiyo ilikuwa imepinga madai kwamba dadake El Aty, Shaimaa Selim ambaye alitoa kanda fupi ya video katika mitandao ya kijamii akidai kwamba dadake aliyekuwa hawezi kuzungumza ama hata kutembea hajapunguza uzani mkubwa kama hospitali hiyo inavyodai.
Daktari wa upasuaji wa watu walionenepa kupitia kiasi Muffi Lakdawala pia alikana madai hayo katika mtandao wa Twitter - bbc swahili

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search