'Mwizi wa Mafuta ya Transfoma' yamemkuta!! apigwa shoti na kupoteza Uhai!
Kijana mmoja anaeshukiwa kuwa muhalifu mwenye umri wa kati
alikuwa na siku mbaya usiku wa kuamkia jana (17/05/2017) baada ya zoezi lake la
kufanya uhalifu kwenye Miundombinu ya Tanesco kutotimia na kumsababishia
kupoteza maisha.
Tukio hili limetokea eneo la Mbagala, Mtaa wa Saku
Ilulu na kuthibitishwa na mafundi wa Tanesco na wapita njia waliofurika eneo
hilo kuangalia mwili wa kijana huyo ambae hakufamika jina lake mara moja akiwa
na majeraha mengi mwilini mwake kuashiria kuunguzwa na shoti wakati wa zoezi
lake lililoishia pabaya.
Kumekuwapo na wimbi kubwa la wizi wa vifaa mbali mbali
na uharibifu wa miundombinu katika transforma za Tanesco maeneo ya Saku katika
siku za hivi karibuni, huku wahalifu wakisemekana kulenga vifaa mbali mbali
zikiwemo ‘fuse’ na mafuta ya transforma na hivyo kusababisha matukio mengi ya kukatika
umeme na kuchochea matukio ya kihalifu kutokana na maeneo mengi ya Mtaa huo kuwa
gizani.
Mkazi mmoja wa Kitongoji cha Saku aliyejitambulisha
kwa jina moja la Baba Ibrahim, nae amethibitisha uwepo wa kadhia ya kukatika
katika umeme mara kwa mara nyakati za usiku katika maeneo hayo… “ni kweli
kabisa ndugu mwandishi,.. matukio ya kukatika umeme mtaani kwetu yamekuwa yakijirudia rudia kila
mara katika siku za hivi karibuni,.. hatua ambayo imesababisha matukio mengi ya kihalifu ikiwemo uvamizi na
wizi”.. alipasha mpashaji ambae ni mkazi wa miaka mingi wa Kitongoji cha
Saku.
Blog yako matukio ilifanikiwa kunasa
picha mbili zinazosemekana ni mwili wa mhalifu huyo ukiwa umeharibika vibaya !
ciaooo...!!
...endelea
kufuatilia blog www.tanzaniampyamatukio.blogspot.com
!
No comments:
Post a Comment