Dk. Kigwa aja na mapya ya ‘makinikinia..' #share.. asema waliposema ‘walikimbizwa kama wezi..’

Mbunge wa Nzega Vijijini, Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ameweka wazi kuwa daima ataendelea kupambana dhidi ya rasilimali za umma, kwani amekuwa mwanaharakati kwa muda mrefu.



“Tuliopinga wizi wa madini yetu tulibezwa, tulikamatwa kama wezi; tuliswekwa ndani, tulionekana wasaliti. Leo kiko wapi? #NasimamaNaRaisWangu” aliandika Dk. Kigwangalla huku watu mbalimbali wakitoa maoni yao.

Kwa mujibu wa Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, suala la kupambana na rasilimali za Taifa alilianza miaka mingi kwani miongoni mwa matukio makubwa ni la 2013, ambapo alijitolea kupambana kudai haki tukio lililopelekea kutiwa nguvuni na Jeshi la Polisi.

Dk. Kigwangalla anasema katika kupigania maslai Taifa ataendelea kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Magufuli mwanzo mwisho kwani ni moja ya matunda ya nchi yoyote ile Duniani.


Anasema kiongozi Mkuu lazima alinde na kupigania rasilimali za nchi, hivyo akiwa Mtanzania na kiongozi mwenye dhamana anaunga juhudi hizo bila kuchoka – CR. JJMSACKY

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search