JPM apiga 'dongo' kiaina.. #share.. Azindua Mtambo wa Maji Ruvu Juu..


Rais John Magufuli leo ameendelea na ziara yake Mkoani Pwani na amefungua kuzindua mtambo wa maji wa Ruvu Juu ambao unasambaza maji katikana mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

Mtambo huo ambao ni wa pili kwa ukubwa baada ya Ruvu Chini umepanuliwa na kuuwezesha kuzalisha maji kiasi cha mita za ujazo 196,000 kutoka kiwango cha mita za ujazo 82,000 ilizokuwa inazalisha zamani.

Maeneo yanayonufaika na mradi huo ni yale yaliyo kandokando ya bomba ambayo ni Mlandizi, Visiga, Kongowe, Kiluvya, Kibamba, Mbezi na Kimara.

Maeneo mengine ni Changanyikeni, Ubungo, Kibangu, Makuburi, Tabata na Segerea.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search