Ziara ya JPM ilivyogeuka 'Limao' kwa Mutalemwa wa DAWASA #share..
Katika ziara ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoendelea katika Mkoa wa Pwani, jana alipata fursa ya kuzindua rasmi mtambo wa kusafisha na kusukuma maji wa Ruvu Juu, Mlandizi mkoani Pwani, shughuli ambayo pia imehudhuriwa na wawakilishi wa Benki ya Dunia, nchi za India na China.
Akiongea katika uzinduzi huo, Rais Magufuli, alieonekana wazi kukerwa na kasi ndogo ya mambo yanavyokwenda ndani ya Dawasa, alimtaka Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo ya Maji Safi na maji taka Dar es Salaam, Archad Mutalemwa kustaafu kwa hiyari yake kwa sababu ameitumikia nchi kwa muda mrefu.
Akaongeza kwamba asisubiri aondolewe kwa kashfa kwa sababu ukifanya kazi kwa muda mrefu, kuna uwezekano mkubwa wa kukwaa kashfa mbalimbali, akasisitiza kwamba faili la Mutalemwa analo mezani kwake na kwamba anamfahamu vizuri.
Kama ulipitwa na hotuba ya Mhe. Rais kwenye uzinduzi huo.. fuatana na maktba ya matukio kupata yaliyojiri..
Akiongea katika uzinduzi huo, Rais Magufuli, alieonekana wazi kukerwa na kasi ndogo ya mambo yanavyokwenda ndani ya Dawasa, alimtaka Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo ya Maji Safi na maji taka Dar es Salaam, Archad Mutalemwa kustaafu kwa hiyari yake kwa sababu ameitumikia nchi kwa muda mrefu.
Akaongeza kwamba asisubiri aondolewe kwa kashfa kwa sababu ukifanya kazi kwa muda mrefu, kuna uwezekano mkubwa wa kukwaa kashfa mbalimbali, akasisitiza kwamba faili la Mutalemwa analo mezani kwake na kwamba anamfahamu vizuri.
Kama ulipitwa na hotuba ya Mhe. Rais kwenye uzinduzi huo.. fuatana na maktba ya matukio kupata yaliyojiri..
No comments:
Post a Comment