Biashara: Dk. Mpango azitaka Taasisis za fedha kulipa kodi, kuepuka mkono wa serikali kuchukua hatua za kisheria dhidi yao..#share.


WAZIRI wa Fedha na Mipango Dk. Phillip Mpango amezitaka Taasisi zote zinazotoa huduma za kifedha nchini kuhakikisha zinalipa kodi stahiki ili kuepuka mkono wa serikali kuchukua hatua za kisheria dhidi yao.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salam wakati ufunguzi wa Kongamano la tatu la huduma za kifedha vijijini ulioandaliwa na Taasisi za Huduma za Kifedha nchini (TAMFI), Mpango alisema taasisi hizo zimekuwa zikitoa mikopo kwa riba kubwa huku hazilipi kodi.

“Kodi hizi ni kwa ajili ya maendeleo ya Taifa, hivyo niwatake wahusika wote wachukue hatua kujirekebisha kabla ya mkono wa sheria haujawafikia,” amesema Dk. Mpango.

Aidha katika mkutano huo ambao unalenga kujadili namna ya kumsaidia mkulima kuweka vivutio vya kiuchumi hususani kwenye mazao ya shambani, Mpango alizitaka taasisi hizo za fedha kuhusisha pia wadau mbali mbali wanaoweza kuongeza thamani za mazao ya kilimo.

Mpango ameziomba kutoa mikopo yenye mashariti nafuu kwa wajasiria mali wadogo na wakati pamoja na kuwapatia elimu ya namna ya kukopa na kuitumia kwa maendeleo ya kiuchumi badala ya kuitumia kwenye anasa pamoja na jinsi ya kuirudisha kwa wakati.

Aidha ametoa rai  kuwa kwa vikundi vyote vyenye rekodi nzuri ya kurejesha mikopo kwa wakati waona umuhimu wa kuwakopesha kwa masharti nafuu ambapo alitoa mfano kwa vikundi vya wanawake ambavyo vina rekodi ya 98% ya kurejesha mikopo kwa wakati.

Amezitaka pia kuwa na tabia ya kufuatilia maendeleo ya miradi ambayo wanaitolea mikopo pasipo kusubiri ife kwani hiyo itawasaidia kujua  changamoto mbali mbali zinazowakabili wakapeshwaji nakuweza kuwasaidia.

Pia ameshauri kuwepo na utaratibu wa kutoa mikopo kwa njia ya teknolojia ya habari mfano kwa njia ya mtandao ambayo inarahisisha katika utoaji wa mkopo kwa mda mfupi hata kwa mtu aliyembali.

Amewahakikishia kuwa serikali itahakikisha panakuwepo na sera nzuri na taratibu za utoaji wa huduma ndogo ndogo za kifedha ambapo alisema sera hiyo itakuwa imekamilika kabla ya mwezi Juni mwakani.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search