Breaking News!! AY na MwanaFA 'waigaragaza' Tigo Mahakama ya Rufaa.. sasa kulamba Bilioni 2.1 fidia.. #share..

Mahakama Kuu ya Tanzania imetupilia mbali rufaa iliyofunguliwa na kampuni ya Tigo kupinga kuwalipa wasanii AY na MwanaFA Tshs 2,185,000,000 kwa kutumia nyimbo zao bila kulipa. 


Wanamuzi Ay na MwanaFA katika pozi.
Wakili Albert Msando ambaye anawakilisha wasanii hao amesema huu ni ushindi muhimu kwa sanaa ya Tanzania. 
Amenukuliwa akisema "ni haki yao kulipwa kwa sababu ni kazi zao ambazo zinalindwa kisheria".
Mdau maarufu wa kwenye tasnia ya Bongo Movie na Bongo fleva, John Seka, akiposti ujumbe mrefu kupitia akauti yake ya FB amempongeza 'Wakili Msomi' Albert Msando kwa kutetea haki ya wasanii hao, akisema ni njia ya mfano kwa wasanii 'chipukizi' wanaoporwa haki zao..

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search