Breaking News: Chadema yapaza sauti kutaka Dk. Mashinji na wenzake waachiliwe haraka.. #share


SEKRETARIETI ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Makao Makuu katika kikao chake cha leo imetoa maazimio manne, likiwemo la kutaka Katibu Mkuu wake, Dk Vicent Mashinji na viongozi wengine 10 waliokamatwa siku mbili zilizopita kuachiwa huru mara moja kabla hakijachukua hatua zaidi.

Katika taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano, Tumaini Makene, Chadema kimetaka Dk Mashinji na wenzake kuachiwa kabla ya hatua nyingine hazijachukuliwa kulinda uhuru na haki za kikatiba na kisiasa zilizoko kwa mujibu wa sheria za nchi.

“Iwapo kesho Jumatatu  mamlaka hizo hazijamwachia huru Dk Mashinji na viongozi 10, chama kupitia kwa mwanasheria Mkuu wake kitatangaza maamuzi yatakayochukuliwa kwenye mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika hiyo kesho,” alisema Makene.

“Katika hatua ya sasa Sekretarieti pia imeelekeza kwa haraka mawakili wa Chama kusimamia kesi dhidi ya Katibu Mkuu na Viongozi wengine kuhakikisha kuwa masuala ya kisheria yanafuatwa na haki kutendeka. Kwa sasa jambo hilo litasimamiwa na Wakili msomi Edson Mbogoro.”


Amesema aidha, Sekretarieti imemteua Katibu ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emanuel Masonga kukaimu kazi za Kanda ya Kusini wakati ambao Mwenyekiti na Katibu wa Kanda hiyo wakiwa mahabusu.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search