Breaking News: Mzee Lowasa 'alivyopamba' Mazishi ya Marehemu Joseph Nkaissery yanayoendelea muda huu Jijini Nairobi.. #share..

Tofauti na ilivyo kawaida wakati huu wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu zinazoendelea zinazotawaliwa na purikushani za hapa na pale,.. hali ya huzuni na utulivu imetawala Jijini Nairobi Nchini Kenya leo kunakofanyika Mazishi ya Kitaifa ya Mwanasiasa Mkongwe na Waziri wa Mambo ya Kiusalama wa Ndani wa Kenya Mwendazake Joseph Nkaissery.


Haya ni Mazishi ya kipekee kufanyika katika siku zaribuni ukizingatia historia ya Mwendazake Nkaisery ambae kabla kuteuliwa kwenye Baraza la Waziri katika Serikali ya Jubilee ya Uhuru Kenyatta, alikuwa mfuasi 'gogo' wa Siasa za Upinzani hususan kambi ya Mgombea urais wa Kenya katika Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni na Waziri Mkuu wa Zamani Bw. Raila Odinga.. 
Miongoni mwa waliohudhuria kutoka nje ya Kenya ni pamoja na Mzee Edward Lowasa kutoka kambi ya Upinzani ambae kama ilivyo kwa Odinga, nae amewahi kuwa Waziri Mkuu katika awamu iliyopita ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete..
Matukio360 imefanikiwa kupata picha kadhaa ya yanayojiri katika mazishi hayo,.. endelea kuwa nasi tuendelee kukujuza..



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search