Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kesho mgeni rasmi kongamano la wanawake waombolezao....#share

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassani anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Kongamano la Wanawake Waombelezao Kitaifa kesho jijini Dar es Salaam.


Mchungaji Deborah Malassy ambaye Mratibu wa kongamano hilo wa kwanza kulia akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu kongamano la Wanawake Waombelezo Kitaifa.

Hayo yamebeinishwa leo jijini Dar es Salaam na Mratibu wa Kongamano hilo Deborah Malassy akizungumza na waandishi wa habari, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwajengea uwezo viongozi wanawake katika kutambua nafasi zao ili kuwawezesha kupata ujasiri wa kuongoza.

“Katika kongamano hili kutakuwa na utoaji elimu kwa wanawake jinsi ya kujilinda na unyonyaji wa kijinsia, kutoa elimu ya ukatili wa rushwa ya ngono na kuwapatia elimu ya njia za kujitambua kiuchumi katika jamii,”amesema Deborah.

Aidha amesema katika kongamano hilo pia watamuombea Rais John Magufuli ili Mungu ampe nguvu katika kuendelea na majukumu yake ya kulinda Taifa, kukuza amani na uchumi wa Nchi.

Mchungaji Deborah amewaomba wanawake kujitokeza katika kongamano hilo ili kuwajengea uwezo wa kiroho, kijamii na kuunda mitandao ya wanawake mbalimbali kutokana na malengo yanayofanana na kuwajengea nguvu ya pamoja.
Na Dalila Sharif





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search