PICHA 23: JPM amfariji Dr. Mwakyembe,.. aendesha harambee kanisani Chato na kufanikiwa kuchangisha Tshs. milioni 13, ahadi Tsh laki 9 na mifuko 33 ya saruji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Leo July 16, 2017  ametuma Salamu za Rambirambi kwa Waziri wa Habari Dkt Harrison Mwakyembe aliefiwa na mkewe Bi. Linah George Mwakyembe aliefariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 15/07/2017 na kuelezea kuguswa kwake na kifo cha Bi Linah.
Wakati huo huo Rais amehudhuria Ibada ya Jumapili ya 15 ya mwaka wa Kanisa iliyofanyika katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita na ameendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo.

Katika harambee hiyo Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amefanikiwa kuchangisha fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni 13, ahadi Shilingi 920,000/=, mifuko ya saruji 33 na malori 2 ya mchanga.














































































About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search