BREAKING: JPM 'atibua' Kata 25 uchaguzi CCM.. Polepole ataja 'dawa' kwa waliboronga.. asema wengine walidiriki kujipangia 'safu za Viongozi wao'.. #share

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), kimesema kitawaita kwenye Kamati ya Madili na kuwahoji wagombea waliovuruga uchaguzi wa ndani kwenye maeneo mbalimbali katika uchaguzi wa ndani unaoendelea nchini na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Katiba yao.

Kauli hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea changamoto zilizojitokeza katika chaguzi hizo.

“Watu hawa wanaoendeleza makundi ndani ya chama chetu ni wasaliti, tunataka viongozi ambao watakitumikia chama na wananchi kwa uadilifu mkubwa, na hii ndiyo dhana ya CCM Mpya,” alisema Polepole.

Alitaja changamoto ambazo zimejitokeza katika uchaguzi huo kuwa ni pamoja na kuwepo kwa makundi ambayo yamekuwa yakipanga safu za viongozi wanaowataka lakini pia baadhi ya maeneo kutowatendea haki wanachama katika upitishwaji wa wagombea.

Polepole alisema kutokana na changamoto hizo Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli na Katibu Mkuu wake walipokea malalamiko na kero za uchaguzi huo kutoka kwa wanachama. Baada ya kuzipokea Mwenyekiti alimwagiza Katibu kufuta chaguzi katika maeneo yaliyokuwa na dosari hizo.

Alitaja kata 24 ambazo chaguzi hizo zimefutwa na kuwa zitarudiwa  kwa kutolewa fomu upya kwa wanachama na kurejeshwa.

Maeneo ni kata za Lumemo-Kilombero, Seriya kwa Vijana-Kondoa, Kariakoo, Liwiti, Manzese, Buguruni, Mianzini, Makuburi, Kigamboni, Gerezani, Segerea, Pugu Stesheni, Pugu, Kitunda, Ukonga, Msasani, Makumbusho, Mabibo na Ndugumbi zote za Dar es Salaam.

Nyingine ni kata za Mapinga- Bagamoyo, kata zote za Simanjiro mkoani Manyara na Mchafukoge.



Na Abraham Ntambara 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search