KIMENUKA: TLS yawataka wanachama wake kususia Mahakama kwa Siku Mbili.. Kisa!? kuomboleza kulipuliwa Ofisi ya Fatma Karume.. #share

BARAZA la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), limewataka wanachama wote wa TLS nchi nzima kususia kuhudhuria katika Mahakama pamoja na Mabaraza ya aina zote kesho kutwa  na Jumatano Agosti 29 hadi 30 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Rais wa TLS Tundulisu lengo likiwa ni kuunga mkono mawakili wa IMMMA Advocates na kuonyesha kutokubaliana kwao na vitendo vya kihalifu vya kuwashambulia mawakili hao kwa mabomu.

Itakumbukwa kuwa usiku wa kuamkia jana Ofisi za IMMMA Advocates zinazomilikiwa na wakili Fatma Karume na Lawrence Masha zilizoko jijini Dar es Salaam ziliungua moto kutokana na shambulio la mabomu.

“Kitendo cha kushambulia Ofisi za IMMMA Advocates kwa mabomu na kusababisha uhalifu wa ofisi hizo ni kitendo cha kigaidi kwa mujibu wa kifungu cha 4(3) cha Sheria ya Kuzuia Ugaidi, 2002,” amesema Lissu.

Amebainisha kuwa kitendo cha kushambulia ofisi hizo kwa mabomu kina lengo la kuwatisha mawakili hao wasiweze kutekeleza wajibu wao kama wanasheria na mawakili kwa kuwatia hofu ya kuwadhuru kimwili au kuwapotezea maisha.

Amesema licha ya kuwataka mawakili kutokwenda kazini katika siku hizo, Baraza hilo limevitaka vyama vya ulinzi na usalama kutumia mamlaka vilivyonavyo ya kuipelelezi kuhakikisha kwamba smabulio hilo linachunguzwa kwa kina ili kuwezesha kujulikana kwa wahusika na kuchukuliwa hatua zinazostahili kisheria dhidi yao.

Lissu ameeleza pia Baraza limevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwahakikishia ulinzi na usalama wa kutosha mawakili wa IMMMA Advocates dhidi ya vitisho au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha usalama wao wa kitaaluma.

Ameongeza kuwa watafanya jitihada za haraka kukutana na Inspekta Jenerali wa Polisi, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) pamoja na Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania ili kujadiliana juu ya shambulio hilo na usalama wa mawakili wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kitaaluma.

Aidha amewataka wananchi kuhakikisha wanalinda usalama, uhuru na heshima ya wanasheria na kuwawezesha mawakili nchini kutekeleza wajibu wao wa kitaaluma wa kulinda utawala wa Sheria na Haki za Binadamu.
Na Abraham Ntambara




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search