Breaking: Spika Ndugai Leo kamalizana na Maalim Seif.. ni hivyo yaani!! #share

SPIKA wa Bunge Job Ndugai amesema hamtambui Maalim Seif kama kiongozi Wa kutekeleza majukumu ya Chama cha Wananchi CUF kwa sasa kutokana na kwamba hafiki ofisini na taarifa alizonazo kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nafasi yake imekaimiwa na Naibu wake Magdalena Sakaya.
Itakumbukwa miezi kadhaa iliyopita Maalim Seif akizungumza na waandishi Wa Habari alimtaja Spika wa Bunge Ndugai kama mmoja wa maadui wanaoendeleza mgogoro wa CUF, alitaja wengine kuwa ni Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, Ofisa ya Usajili ya Vizazi na Vivo (RITA) na kadhalika.
Kauli hiyo Ndugai ameitoa jioni hii wakati akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari alipotakiwa kitoa kauli kwa kutajwa na Maalim kama mmoja wa maadau wa Chama cha CUF, amesema tangu Machi mwaka huu alipokea taarifa ya Msajili kuwa kiongozi huyo anamuda hajafika ofisini.
"Mimi watanzania wrote ni ndugu zangu na sichukii Chama chochote, na kunapotokea suala la utaratibu ni kufuata utaratibu tu,"
"Mwezi Machi mwaka huu nilipokea taarifa kutoka kwa Msajili kwamba Kuna taarifa Maalim ana muda hayupo ofisini na majukumu yote yatakuwa chini ya Naibu wake," amesema Ndugai.
Aidha amefafanua kuwa huo ndiyo msimamo uliopo na kwamba hats akiletewa taarifa kutoka kwa Kiongozi Hugo Wa CUF hawezi ifanyia kazi hadi apate taarifa kama amekwisharudi ofisini.
" sasa kama ni wewe umeletewa taarifa kama hiyo na Msajili ungefanyaje, maana masuala yote ya Vyama hata kunapotokea sintofahamu ndani ya vyama nachofanya ni kupata taarifa kutoka kwa Msajili," amesisitiza.
Amewashauri CUF kusafisha nyumba yao wenyewe na kuacha kkulaumu watu wengine na kusisitiza  kwa kuwa Ofisi ya Msajili haimtambui na yeye hawezi kumtambua, anayetambuliwa kwa sasa aliyechua majukumu take ni Sakaya

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search