Breaking: Tundu Lissu atoka rumande jioni hii baada kukamilisha masharti ya dhamana.. #share

Mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa chadema Tundu Lisu ameachiwa huru kwa dhamana.

Akizungumza mara baada yakutoka nje ya kituo kikuu cha polisi wakili wake  Peter Kibatala amesema Lisu ameachiwa kwa dhamana na atatakiwa kurudi tena tare 28 siku ya jumatatu.
Baada ya kutoka nje ya kituo cha polisi Lisu hakutakiwa kuzungumza chochote kutokana na masharti ya dhamana badala yake aliingia moja kwa moja kwenye gari ya wakili wake.

Kibatara amesema Lisu anatuhumiwa kutoa maneno ya uchochezi pamoja na  kumkashfu Rais.

Lisu alikamatwa Jumanne wakati akitoka Mahakama ya hakimu mkazi kisutu alipowenda kwaajili ya kesi pamoja na kumtetea mteja wake.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search