Chadema yatangaza Mgogoro dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Momba Juma Irando....#share

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza
mgogoro na mkuu wa wilaya ya Momba mkoni Songwe, Juma Irando kwa kuagiza jeshi
la polisi wilayani humo kumuweka ndani kwa saa 48 mbunge wa Jimbo la Tunduma,
Frank Mwakajoka kwa madai ya uchochezi.
Mgogoro huo umetangazwa leo na Mwenyekiti wa chama hicho katika Halmashauri
ya mji wa Tunduma Ali Mwafongo akizungumza na waandishi wa habari, ameleezea kusikitishwa na amri hiyo ya mkuu wa
wilaya na kusema kuwa kamwe hawatarudi nyuma huku akiahidi kutompa ushirikiano
mkuu wa wilaya huyo.
“Viongozi wetu wamekuwa wakipelekeshwa sana lakini katu
hatutokata tamaa kwa sababu ni kazi yetu kusema ukweli na kuwatumikia wananchi
wetu,"
"Uchungu tunaopata tunajua ipo siku itakuwa furaha kwetu
kwani ushindi unakaribia. Kinachofanywa sasa hivi wakumbuke ipo siku watawala
watakuwa wapinzani na haya yanayofanywa hayataweza kuturudisha sisi nyuma,” amesema
Mwafongo.
Aidha mbali na agizo hilo mkuu huyo wa wilaya pia ametuhumiwa kutoa amri
ya kushusha bendera za Chadema hali ambayo imeonesha kuwakera viongozi wa chama
hicho.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Irando amekiri kutoa amri ya kukamatwa
kwa mbunge huyo kwa madai kuwa ametoa kauli ya kudharau mamlaka ya uteuzi.
Mbunge Mwakajoka amekamatwa jana Jumanne na kuwekwa ndani
ikiwa ni siku moja tu baada ya Mbunge mwingine wa Jimbo la Vwawa, Paschal
Haonga kukamatwa na jeshi la polisi.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment