Mwigulu Nchemba atoa rai Jumuiya kuwaita na kuwahoji wanaoichafua Tanzania kufukuza wakimbizi wa Burundi...#share

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba ametoa rai kwa wadau wa Jumuiya zinazoshughulikia wakimbizi kama Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Dunia (UNHCR) kuita na kuwahoji watu watakaoendelea kusambaza taarifa za uzushi kuwa Tanzania inafukuza wakimbizi wa Burundi nchini  ili kudhizibitisha.



Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Nchemba akifungua mkutano wa wadau wa Jumuiya ya Wakimbizi wenye lengo la kujadili na kuweka mipango mizuri ya jinsi ya kuwarudisha Burundi wakimbizi waliojiorodhesha kwa hiari yao  kurudi nchini kwao.

Amesema kumekuwepo na baadhi ya vyombo vya kimataifa ambavyo vimekuwa vikidhani kuwa Tanzania inataka kuwaondoa wakimbizi hao kwa nguvu ya majeshi suala ambalo siyo sahihi.

Amefafanua kwamba sababu ya kusemwa hayo inatokana na vurugu zilizoanzishwa na wakimbizi wenyewe katika kambi wakishinikiza Jumuiya za Wakimbizi kuharakisha mchakato wao wakurudi nchini Burundi kwa ajili ya kuwahi msimu wa kilimo.

Amesema vurugu hizo zilipelekea uharibifu wa mali za wananchi wa jirani na kambi hivyo ikabidi polisi kuingilia kati kuwatuliza ndiyo ikachukuliwa kama Tanzania wanataka kuwaondoa kwa nguvu.

“Nimeona hili niliweke sawa kabisaa maana kuna baadhi ya vyombo vya nje walizani Serikali inafukuza wakimbizi, kwanzia sasa atakeyeendelea kutoa taarifa hizo ili kuichafua Tanzania, niombe jumuia ya wadau wa wakimbizi iwaite mizani waeleze wanavyofukuzwa,” amesema Nchemba.

Aidha amebainisha kuwa hali hiyo ya vurugu ilitokea baada ya  Agosti 22 Rais wa Burundi  Pierre Nkurunziza kukutana na Rais John Magufuli na kumhakikishia kuwa kwa sasa hali ya Burundi iko shwari na kwamba wanaweka mipango sawa ili kuwapokea wakimbizi ambao wako tayari kurudi nyumbani kujenga nchi yao.

Waziri Nchemha amesma hadi sasa zaidi ya wakimbizi 12,000 wamekwisha jiorodhesha kutaka kurudi nchini Burundi ambapo waataanza kurudishwa Septemba 7 mwaka huu na kutakuwa na mwendelezo hadi wote waliotayari kurudi watakapokwisha.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Burundi Pascal Barandagiye, amesema wakotayari kuwapokea wananchi wao. Na amewahakikishia kuwa hali iko shwari na kuwataka waendelee kujiandikisha kwa wingi.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search