GUMZO: Buda kajiua baada ya kura za Boss wake kutotosha kwenye nafasi ya Ugavana Nchini Kenya.. #share

Wahenge wetu husema... Siasa ni 'mchezo wa rafu'.. Maneno haya ya Wahenga yalithibiti jana Nchini kenya baada ya Bwana mmoja wa makamo kuamua kujimaliza mwenyewe kufuatia kushindwa Uchaguzi kwa mtu aliemtegemea sana kushinda katika Uchaguzi Mkuu uliopita.


Taarifa iliyochapishwa na Mkuu wa Polisi Wilayani Nyandaruwa nchini humo Kamishna Msaidizi  
Timon Odingo, mwendazake  huyo David Mathenge, mwenye umri wa miaka 51,.. aliacha ujumbe wa maandishi ukielezea sababu kuu ya kujiua kwake kuwa ni hali kutamaushwa kulikotokana na Gavana wa Leikipia MHE.Joshua Irungu kupoteza kiti chake, licha ya kampeni kubwa waliyoifanya..  
Kumerikuwa na visa na mikasa Nchini kenya tokea Kamishna mkuu wa Tume inayosimamia Uchaguzi na Mipaka Bw. Ezra Chiloba kutangaza matokeo yualiyomuonyesha Bw. Uhuru Kenyatta akimtupa mbali mpinzani wake mkuu Bw. Raila Odinga katika matokeo ya mwisho ya kura za urais.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search