sPORTS nEWS: StarTimes RBA yaja na All Star wiki hii....#share
KAMPUNI ya StarMedia Tanzania Limited ambao ni Wadhamini Wakuu
wa ligi ya kikapu ya RBA, wanataarajia kuleta mechi ya All Star mwishoni mwa
wiki hii ambayo itashirikisha wachezaji vinara katika ligi hiyo.
Taarifa iliyotumwa leo kwa vyombo vya habari na Kitengo cha
Mahusiano cha Kampuni hiyo kilibainisha kuwa mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa siku ya Jumamosi Septemba
2 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo imesema kuwa baada ya kuanza kwa
hatua ya robo fainali (playoffs), wapenzi wa mpira wa kikapu jijini Dar es
Salaam na Tanzania Kwa ujumla watapata nafasi ya kushuhudia wachezaji vinara wa
ligi hiyo wakiwapatia burudani kupitia
mchezo huo.
Mchezo utahusisha timu mbili ambazo zimepewa majina ya NYOTA
na MAMBO, majina ya vifurushi vya gharama nafuu vya StarTimes, ndizo zitashuka
dimbani katika uwanja wa Ndani wa Taifa ili kutoa Burudani ya aina yake kwa
watazamaji.
Mchezo unatarajiwa kupigwa kati ya saa 2 hadi saa 4 Usiku,
Lakini kabla ya mchezo kuanza kutakuwa na michezo kadhaa ya utangulizi na
Onyesho kutoka kwa Msanii Jay Moe.
Mchezo wa All Star ni sehemu ya ufunguzi kwa hatua ya Mtoano
(PlayOffs) ambayo itahusisha jumla ya timu nane (8), ili kumpata mshindi na
timu tatu (3) zitakazopata nafasi ya kushiriki ligi ya Taifa hapo baadaye mwaka
huu. Hatua hiyo inatarajiwa kuanza tarehe 6 Septemba.
Akizungumzia muendelezo wa ligi hiyo Meneja Mahusiano wa
Kampuni ya StarTimes, Juma Suluhu amesema kuwa kampuni hiyo itaendelea kusaidia
ukuaji wa michezo nchini ikiwa ni sehemu ya Uhusiano mzuri kati ya kampuni hiyo
na Watanzania.
“Tunajisikia fahari kuchangia kuinua vipaji kwa vijana wa
kitanzania kupitia mpira wa kikapu ambao pia una wapenzi na washiriki wengi
hivyo udhamini wetu unakuwa ni sehemu ya shughuli nyingi za kijamii ambazo
kampuni yetu inaendelea kufanya” alisema Juma.
Ligi ya StarTimes RBA inaonyeshwa MUBASHARA kila siku za
Ijumaa, Jumamosi na Jumapili kupitia Chaneli ya Sibuka Maisha ambayo
inapatikana katika king’amuzi cha Startimes, kwa gharama ya Tshs 3000 kwa
Mwezi.
Mbali na ligi RBA StarTimes ndiyo kampuni yenye kibali cha
kuonyesha michuano ya Mpira wa kikapu Kimataifa (FIBA), na sasa wanaendelea
kuonyesha ligi ya Kikapu kwa Wanawake AfroBasket inayochezwa nchini Mali.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment