nEWS: TIC yavunja rekodi usajili miradi ya uwekezaji, pia ya zalisha ajira kwa watanzania....#share

KITUO cha Uwekezaji (TIC) kimesajili hadi sasa miradi 209 kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Julai mwaka huu ambayo inategemewa kuzalisha ajira rasimi na zisizo rasmi zaidi ya 12,452.


Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geofrey Mwambe akizungumza na waandishi wa habari, alisema kiwango hicho ni kikubwa ukilinganisha na mwaka uliopita ambapo walisajili miradi 306 tu.

“Hadi sasa tumekwisha sajili miradi 206 kwa kipindi cha miezi saba, hii inamana kwamba tunaeza kusajili miradi mingi zaidi kwa muda huu uliobaki kabla ya mwaka huu kumalizika,” alisema Mwambe.

Aidha alisema wameandaa mpango maalum wa Mfuko wa Benki ya Ardhi ambao utasaidia katika kurahisisha upatikanaji wa ardhi  na kuleta ufanisi katika upatikanaji wa maeneo ya ujenzi wa viwanda pamoja na uwekezaji mwingine.

Alisema hadi sasa maeneo yaliyopatikana kwa ajili ya ujenzi wa viwanda ni Kigamboni na Tanga na wanategemea kuongezeka kwa mitaji ya kutoka nje na ndani yaani FDI na DD1 kutokana na kupata miradi mikubwa Sita.

Mwambe alifafanua kuwa miradi hiyo yenye hadhi ya kimkakati iliyosajiliwa na TIC na kupitishwa na Baraza la Taifa la uwekezaji. alisema miradi hiyo kwa pamoja inategemewa kuwekeza zaidi ya dola za kimarekani sh. bilioni 2.626 na inatarajiwa kuzalisha  kiasi cha ajira 13,885 ambazo zitanufaisha watanzania.

alieleza kuwa juhudi za uhamasishaji ujenzi wa viwanda zimeweza kuzaa matunda na mpaka sasa wameweza kusajili viwanda vikubwa ambavyo vitasaidia katika kubadilisha hali ya uchumi wa nchi.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search