nEWS: Mahakamani Kisutu, Waanzilishi wa Jamii FORUMS wakana mashtaka dhidi yao......#share

MKURUGENZI wa Kampuni ya Jamii Media Limited, Maxence Melo na mmiliki mwenza wa kampuni hiyo Mike William leo Mahakamani Kisutu wamekana maelezo waliyosomewa ya kulizuia Jeshi la Polisi kuuchunguza mtandao huo.

Melo na William wamekana hayo baada ya kusomewa maelezo ya awali na Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa katika kesi ya kulizuia Jeshi la Polisi kuuchunguza mtandao wao kwa kuchapisha taarifa za uongo.

Katika maelezo hayo, Melo na William wamekubali wasifu wao, ikiwemo majina, umri, kumiliki mtandao wa Jamii Forum na kukamatwa kisha kufikishwa Mahakamani lakini hata hivyo, wamekana kuhusika na tuhuma za kulizuia Jeshi la Polisi kuuchunguza mtandao huo.

Baada ya kusomewa maelezo hayo,
Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi August 24, 2017 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.

Katika kesi hiyo inadaiwa Melo na William walizuia Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi kinyume na Sheria Namba 22 (2) cha Sheria ya Makosa ya Mtandao huku ikidaiwa kati ya May 10 na December 13, 2016 maeneo ya Mikocheni, Kinondoni, walilizuia Jeshi hilo kufanya uchunguzi baada ya kuchapishwa taarifa za uongo dhidi ya kampuni ya CUSNA Investment na Ocean Link.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search