nEWS: Mashirika ya kiraia yatoa tamko kwa serikali kuhusu uhakiki wa NGOs nchini...#share
WAKURUGENZI
wa mashirika yasiyo ya kiserikali sambamba na Baraza la Taifa la Mashirika
yasiyo ya Kiserikali (Nacongo) na Mtandao wa Mashirika ya Kutetea Haki za
Binadamu Tanzania (THRDC) wameunga mkono mchakato wa Serikali kuhakiki orodha
ya mashirika hayo nchini.
Hivi
karibuni serikali ilitangaza mchakato wa uhakiki wa mashirika yote kuanzia Agosti
21 hadi 31 mwaka huu, lengo likiwa ni kuboresha orodha ya mashirika hayo na
kupima utekelezaji wa majukumu yake.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo, mratibu Taifa wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema wanaamini endapo zoezi
hilo litafanyika vizuri litaleta manufaa kwa Taifa.
“Tunaweza
kujua idadi halisi ya mashirika yanayofanya kazi na baadae kujua mchango wa
mashirika hayo kwa Taifa letu kiuchumi na kijamii,” alisema Olengurumwa.
Amesema
mchakato huo pia utasaidia kuondoa kwenye orodha mashirika yaliyoshindwa
kuendelea kufanya kazi nchini na kubaki yale yenye tija tu.
Amebainisha
kuwa kwa muda mrefu mchango wa asasi za kiraia haitambuliwi kitaifa pamoja na
kwamba sekta hiyo hutoa ajira kwa watanzania wengi, kuchangia makusanyo ya
kodi.
Naye
katibu wa Nacongo, Ismail Suleiman amesema kutokana na mchakato huo, baraza
hilo linashauri mashirika hayo kulipa
uzito suala hilo kwa kujitahidi kufika mapema katika ofisi za kanda
zilizopangwa ili kufanya uhakiki katika muda uliowekwa.
Aidha
ametoa rai kwa wasajili wasaidizi kote nchini kuhakikisha kuwa wanaanza kutoa
barua za utambulisho kadri azaki zitakavyokuwa zikiomba kupewa barua hizo. Hiyo
itayawezesha mashirika kujiandaa mapema na zoezi hilo.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment