sPORTS nEWS uLAYA: Wakati jioni hii Manchester United ikitarajia kushuka dimbani dhidi ya West Ham United, Neville hana imani na Lukaku...#share

Gary Neville bado ameonyesha kuwa na wasiwasi  kwa mshambuliaji Mpya wa Klabu ya Mancester United Romelu Lukaku kama anauwezo wa kufanya vizuri katika mechi kubwa.


“Romelu Lukaku lazima awe mchezaji ambaye anatakiwa kuisaidia Manchester United kushinda katika michezo migumu na mikubwa Old Trafford msimu huu,” amesema Neville.

Lukaku alijiunga na  Manchester United akitokea  Everton kwa £75 million Julai mwaka huu na kufanikiwa kufunga goli kwenye mechi dhidi ya  Real Madrid katika kombe la ikikombe cha ligi Ulaya Jumanne iliyopita (Super Cup).

Mbelgiji huyo alifunga magoli 25 msimu uliopita akiitumikia klabu ya Everton huku akiwa ni mpachika nyavu wa pili nyuma ya Mshambuliajia wa Tottenham Harry Kane katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu.

Lakini Neville bado amekuwa na maswali dhidi yake kwani amekuwa akimtazama kwa ukaribu tangu alipowasili nchini Uingereza mwaka 2011.
 “Wasiwasi wangu dhidi yake ni kwamba nimekuwa nikimtazama kwa miaka kadhaa iliyopita akicheza katika mechi kubwa na kwa wakati fulani sidhani kama amaweza fanya vizuri vya kutosha,” Neville amesema  hayo Sky Sports.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search